HABARI MPYA LEO  

WOLPER: Niko fiti kumchakaza Wema!

By Unknown - Jul 6, 2012

HII ni burudani nyingine ya aina yake ambayo itapatikana katika tamasha la Usiku wa Matumaini litakalofanyika Julai 7, Uwanja wa Taifa jijini Dar. Nazungumzia mpambano wa masumbwi kati ya mashostisto wawili maarufu Bongo, Jacqueline Wolper na Wema Sepetu, ebwana eee! Haijawahi kutokea.


Kamera yetu hivi karibuni iliwanasa mwanadada Wolper na bondia Rashid Matumla wakila tizi kwa nguvu zote, pande za Mbezi Beach yalipo maskani ya Wolper, ikiwa ni maandalizi ya pambano hilo litakalokuwa na raundi sita. Wolper alipoulizwa kulikoni amevaa gloves na kusukuma punching bag kama hana akili nzuri, alifunguka kuwa anajiandaa kumchakaza Wema.

“Natafuta pumzi na stamina ya kutosha, si unajua mbele yangu kuna pambano kali dhidi ya adui yangu Wema. Nataka nimshikishe adabu ili tuheshimiane,” alisema Wolper na kuendelea kurusha makonde hewani. Wawili hao waliwahi kuwa mabest lakini baadaye wakatibuana vibaya na kuanzisha bifu linaloendelea hadi leo. Kocha wa Wema ni Maneno Oswald ‘Mtambo wa Gongo’.

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII