March 13, 2025
 

HABARI MPYA LEO  

NAFASI ZA KAZI

SENIOR PLANNING OFFICER      Qualifications: Bachelor’s Degree in Economics, Statistics, Planning, Bu...

Published by Admin

ACADEMIC NEWS AND SELECTION

TUMAINI UNIVERSITY MAKUMIRA (TUMA) FIRST LIST OF ADMITTED STUDENTS INTO VARIOUS PROGRAMMES AT (TUMA) 2012- 2013 INTAKE 1. Th...

Published by Admin

MAKALA MBALIMBALI

Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE ...

Published by Admin

MICHEZO NA BURUDANI

Mshambulizi wa timu ta taifa ya soka ya Uganda Cranes, Uganda, Robert Ssentongo, ameteuliwa kuwa mchezaji bora wa mashindano y...

Published by Admin

Okwi mchezaji wa Simba!

By Unknown - Jul 6, 2012

MASHABIKI wa Simba jana waligeuka 'mbogo' kwa Makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo, Geofrey Nyange 'Kaburu' wakitaka kujua ukweli kuhusiana na tetesi za mshambuliaji wao tegemeo, Emmanuel Okwi kujiunga na Yanga.

Mashabiki hao waliojitokeza kwa wingi makao makuu ya klabu hiyo Mtaa wa Msimbazi walimzonga Kaburu wakati anatoka kwenye mkutano na vyombo vya habari kukanusha taarifa za Okwi kwenda Yanga.

Kaburu aliwatoa hofu mashabiki hao kwa kuwaambia Okwi bado ni mchezaji wao na wasiwe na wasiwasi na kuingia kwenye gari yake aina ya Noah na kufunga vioo na kuondoka.

Kitendo hicho kiliwafanya mashabiki hao kutoa maneno ya vitisho kwa kiongozi huyo kwa kudai hawatakubali kuona Okwi anakwenda Jangwani bila ya maelezo ya maana kutoka kwa viongozi wao wa Simba.

"Kaburu usituzingue kabisa, Yondani (Kelvin) mlituambia hivyo hivyo, tunakwambia kabisa kama Okwi atacheza Yanga hapatatosha hapa," alisikika shabiki mmoja akiongea kwa hasira.

Awali akizungumza na Wanahabari, Kaburu alisema mkataba wa Okwi utamalizika mwakani mwezi Juni na hivi sasa Okwi yupo nyumbani kwao Uganda akijianda kwa safari yake ya kwenda Italia kwa majaribio keshokutwa.

Kaburu alionyesha mkataba aliosaini Okwi wa kuichezea Simba mwezi Novemba mwaka jana ambao unaonyesha mkataba huo utalimalizika Juni 13 mwaka ujao.

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII

Pages 22123456 »