HABARI MPYA LEO  

Sumatra yaweka ukomo umri wa madereva

By Mhariri - Aug 29, 2012

MAMLAKA ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), imesema umri wa madereva wa Usafiri wa Umma unapaswa kuanzia miaka 30 hadi 60 ili kuepusha ajali za mara kwa mara.

Hatua hiyo imekuja wakati kukiwa na matukio mengi ya ajali ambazo zinahusishwa na uzembe wa madereva na kutozingatia sheria za barabarani.

Hayo yalibainishwa Dar es Salaam jana na Mkurugenzi wa Udhibiti Usafiri wa barabarani, Aron Kisaka wakati akiwasilisha Kanuni za leseni ya usafirishaji kwa magari yanayotoa huduma ya usafiri wa umma ya mwaka 2012 kwa wadau wa usafiri.

Vipengele vingine vilivyo wasilishwa katika Kanuni hizo ni pamoja na dereva kutoruhusiwa kuendesha gari zaidi ya saa nane mfululizo, kuendesha gari huku akiongea na simu pamoja na kuendesha gari huku akiwa ametumia kilevi cha aina yoyote.

SOMA ZAIDI KWA KUCLICK HAPA: GAZETI LA MWANANCHI

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII