HABARI MPYA LEO  

Chadema na CUF waungana kuikataa bajeti

By Unknown - Jun 18, 2012



MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba ameungana na wenyeviti wa vyama vingine vya siasa vya upinzani kupinga Bajeti ya Serikali ya 2012/2013, akisisitiza kuwa kamwe chama chake na wabunge wake, hawataiunga mkono.

Lipumba aliiponda Serikali akisema kuwa nchi inahitaji uongozi wenye uwezo wa kusimamia rasilimali za nchi na matumizi ya fedha za umma.

Aliikosoa Serikali akisema imeshindwa kubuni vyanzo vipya vya mapato huku kukiwa na udhaifu mkubwa katika usimamizi wa matumizi ya fedha za umma zinazokusanywa kutoka katika vyanzo vya mapato vilivyopo.

Kwa kauli hiyo, Lipumba ameungana na wenyeviti wenzake wa vyama vya upinzani, Freeman Mbowe wa Chadema na James Mbatia wa NCCR-Mageuzi ambao pia waliiponda Bajeti hiyo wakisema haina jipya.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti baada ya kuwasilishwa kwa Bajeti hiyo Alhamisi usiku, wenyeviti hao walisema hakuna matumaini kwa Watanzania kupitia Bajeti hiyo kwani fedha nyingi zimelundikwa kuwanufaisha wachache huku umma ukiambulia patupu.

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII