HABARI MPYA LEO  

Tangazo muhimu kwa watumia mita za LUKU nchini

By Mhariri - Aug 29, 2012

Kwa niaba ya TANESCO na kwa faida ya wasomaji wangu wa Maganga Media, nimesikiliza kipindi cha TANESCO na MAENDELEO kinachorushwa na TBC1 leo asubuhi na kukutana na taarifa hii ambayo sidhani kama kila mtu anayo.

Ni kuwa TANESCO wameamua kuboresha system ya mita za luku kote nchini kuanzia Tarehe moja Septemba. Kwa mteja wa TANESCO anayetumia mita ya LUKU anatakiwa kama luku yake itaisha baada ya Tarehe 1.9.2012 ANATAKIWA KWENDA KUNUNUA LUKU KATIKA VITUO VYA MAUZO YA LUKU VYA TANESCO ili alipie luku yake. Hapo atapewa risiti 3, Mbili zikiwa ni za utambuzi na marekebisho ya mfumo wa LUKU na hiyo ya 3 ndio ya TOKEN (Umeme ulionunua). Zingatia uende kwenye kituo cha TANESCO, sio lazima uende ofisini, vipo hata mitaani kwa miji mikubwa vimeandikwa TANESCO OFISI YA MALIPO.

Kwa mujibu wa mzungumzaji wa kipindi hicho, sio kwamba wanasitisha njia zingine za kununua umeme kama kwa kupitia njia ya simu, ATM, MAX, na njia nyingine unazoona ni rahisi kwako, bali wanaboresha tu kwa ajili ya manufaa. Mteja kwa mara ya kwanza kuanzia mwezi wa tisa tarehe mosi akinunua umeme kwa njia nyingine umeme huo hautasoma kwenye mita yako ya LUKU. Ukienda TANESCO umeme huo uliolipia utarudishiwa (pesa yako haipotei) ila kukwepa usumbufu, ni bora ukanunue katika ofisi za mauzo za TANESCO.

Ushauri alioutoa ni kuwa si lazima wote mkimbie na kwenda ofisi za TANESCO ifikapo tarehe moja, ila kama utakuwa na UNITS zako utaendelea kutumia hadi zitakapoisha. Muhimu ni yeyote atakayenunua UNITS ZA LUKU kuanzia tarehe moja akanunue katika vituo vya malipo vya TANESCO. Baada ya hapo ndipo utaendelea na utaratibu wako wa kununua katika njia uliyozoea wewe kama ni, ngoja nizitaje kwa hisani yao, (siwapigii debe wenye mitandao hiyo, ni kwa faida ya jamii) kuna MPESA, TIGO PESA, NMB ATM NA NMB MOBILE, MAXCOM, NK.

MAULIZO: 0768 985 100, 022 219 4400
 
KWA MASWALI TEMBELEA KITUO CHA TANESCO KILICHO KARIBU NA WEWE. KAMA BADO KUNA KITU HUJAKIELEWA VIZURI, INGIA KWENYE SANDUKU LA MAONI HAPA CHINI NA ULIZA SWALI LAKO UTAJIBIWA. HII ITAKUSAIDIA SANA KULIKO KWENDA OFISINI MOJA KWA MOJA WAKATI MAJIBU YAPO. Mwisho wa TANGAZO.

TANESCO, wanayaangaza maisha yako!

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII