HABARI MPYA LEO  

Bajeti ya Serikali yapita!

By Unknown - Jun 24, 2012

WAZIRI wa Fedha, Dk. William Mgimwa ‘amewakuna’ wabunge wa Bunge la Tanzania baada ya kuwajulisha kuwa Serikali imekubali mapendekezo yao mengi waliyotoa wakati wanachangia bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2012/2013.

Miongoni mwa mapendekezo ya wabunge yaliyokubaliwa ni kuongeza kima cha chini cha mapato ya wafanyabiashara yanayotozwa kodi kutoka shilingi milioni tatu hadi milioni nne.

Dk. Mgimwa amelieleza Bunge kuwa, uamuzi huo wa Serikali utawawezesha wafanyabiasha wadogo wakiwemo waendesha ‘bodaboda’ kujiendeleza kibiashara.Serikali yetu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ni sikivu…Serikali ni sikivu kwa wabunge wote” amesema Dk. Mgimwa wakati anajibu hoja za wabunge waliochangia bajeti hiyo.

Amewaeleza wabunge kuwa, Serikali pia imekubali ushauri wao wa kuongeza kodi ya mafuta kwa mafuta yanayoagizwa kutoka nje ili kulinda viwanda vya ndani. Kwa mujibu wa Waziri Mgimwa, uamuzi huo wa Serikali sasa utawasilishwa kwenye Baraza la Mawaziri na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki(EAC).

“Lakini Serikali imekubali mapendekezo ya waheshimwa wabunge” amesema. Kwa mujib wa Waziri Mgimwa, Serikali kuondoa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwa viwanda vinavyozalisha nguo kwa kutumia pamba inayolimwa nchini. “Tumeikubali hiyo hoja, tunaifanyia kazi” amelieleza Bunge na kubainisha kwamba, uamuzi huo utasaidia kuongeza ajira nchini na mapato ya wananchi.

Amesema, Serikali inafanya uchambuzi wa suala hilo ili kuona ni wapi itafidia , nakwamba, itatoa ufafanuzi wa jambo hilo katika Muswada wa Fedha wakati wa Mkutano unaoendelea wa Bunge mjini Dodoma.

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII