HABARI MPYA LEO  

Arsenal 3 Norwich 3

By Maganga Media - May 5, 2012


Yossi Benayoun
Bao la kusawazisha la Steve Morison, mchezaji wa Norwich, limepunguza matumaini ya Arsenal, ikichezea uwanja wa nyumbani wa Imarati, kufanikiwa kushiriki katika michuano ya klabu bingwa barani Ulaya msimu ujao. Mechi hiyo ilikwisha kwa sare ya 3-3. Katika kipindi cha dakika moja, Yossi Benayoun tayari alikuwa ameifungia Arsenal bao, lakini kipa Wojciech Szczesny akamruhusu Wes Hoolahan kusawazisha.

Grant Holt aliiwezesha Norwich kufunga bao la pili na kuipatia timu hiyo matumaini ya kupata ushindi, lakini Robin van Persie akatandika mkwaju ambao kipa kabisa hakuwa na nafasi ya kuupata mpira.Bao la Morison katika dakika za mwishomwisho ziliwawezesha kuondoka na pointi moja.

Matokeo hayo yanamaanisha Arsenal imecheza mechi nne za mwisho pasipo kupata ushindi, na kuipunguzia matumaini ya kumaliza ligi katika nafasi ya nne bora kuiwezesha kushiriki katika mechi za klabu bingwa barani Ulaya.

Hatma ya Arsene Wenger na vijana wake wa Gunners, na ambao wamo katika nafasi ya tatu, huenda ikabadilika kufuatia matokeo ya mechi za Jumapili, wakati wapinzani wao wa kaskazini mwa London, Tottenham, watakaposafiri kucheza na Aston Villa, huku Newcastle nao wakiikaribisha Manchester City.

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII