HABARI MPYA LEO  

Muamba alifariki kwa dakika 78

By Maganga Media - Mar 21, 2012


Fabrice Muamba ''alifariki'' kwa dakika 78 baada ya kuzirai uwanjani, amebainisha daktari wa klabu yake ya Bolton Wanderers' Jonathan Tobin.
Madaktari wanasema kua bado ni mapema kutabiri kama atarejea uwanjani kucheza soka. Lakini Dr Tobin amesema ameshangazwa na jinsi mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 alivyoweza kuponyoka hadi wakati huu. Katika mahojiano yenye makiwa, Dr.Tobin amesema hatukua na hakika, fikra zetu ziliwaza mengine kabisa hatukutazamia kufikia hali hii ya afuweni kiasi hiki. Ni ajabu.
 
Muamba alizirai kutokana na kukwama kwa mishipa ya moyo wakati wa mchuano wa Kombe la FA kwenye uwanja wa White Hart Lane jumamosi iliyopita. Dr Tobin ameiambia BBC Michezo kua muuguzi wa klabu ya Bolton Andy Mitchell alikua wa kwanza kutambua kua mchezaji huyo amezirai. Nilimsikia akipiga kelele, ''Nendeni uwanjani,nenda uwanjani'' Hapo ikawa wazi kua kuna hatari pale uwanjani.
 
Alisema kua Muamba alipewa vifaa viwili vya kumsaidia kuikunjua mishipa ya moyo mara ya kwanza uwanjani mara ya pili wakati akipitishwa uwanjani na mara nyingine 13 kwenye gari la wagonjwa kuelekea hospitali lakini ajabu ni kwamba hakuna hata moja lililofanikiwa. Moyo wa Muamba ulipoteza mapigo na kwa mda wa dakika 78 hakupumuwa.
 
Saa mbili baada ya leo kurejesha fahamu, nilimsogelea na kumuuliza jina lake, akajibu,Fabrice Muamba. Nikasema nasikia wewe ni mchezaji mzuri wa mpira' akasema'Najitahidi' Nilijihisi chozi likinitoka.'' Mtaalamu ameongezea kusema kua: "singependa kuahidi muujiza kwa wakati huu lakini kwa hali ilivyo maisha yake hayamo hatarini tena.
 
Bado ni mapema mno kusema kwa uhakika kama atarudi kucheza mpira au la.

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII