HABARI MPYA LEO  

Marekeni kuondoka Afghanistan 2014

By Maganga Media - Mar 18, 2012


Rais Barrack Obama wa Marekani na mwenzake wa Afghanistan Hamid Karzai

  • Jina la mwanajeshi aliyeuwa raia 16 huko lafichuliwa

Rais wa Marekani Barrack Obama na mwenzake wa Afghanistan Hamid Karzai wamethibitisha kwamba majeshi ya Marekani yataondoka nchini humo mwishoni mwa mwaka 2014.
Hatua hii imechukuliwa licha ya miito ya kutaka jeshi la Marekani kuondolewa nchini humo mapema. Marais hao ambao waliozungumza kwa njia ya simu walisisitiza kwamba wataendelea na utekelezaji wa utaratibu wa Lisbon ambapo majeshi ya Afghanistan yatakamilisha hatua za mpito na kuchukua jukumu la usalama nchini humo ifikapo mwishoni mwa mwaka 2014.

Jina la Mwanajeshi lafichuliwa

Huku hayo yakiarifiwa, afisa mmoja nchini Marekani amesema Robert Bales mwenye umri wa miaka 38 ndiye mwanajeshi anayeshutumiwa kwa mauaji ya raia 16 wa Afghanistan. Robert Bales ameoa na ana watoto wawili.

Source: DW

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII