HABARI MPYA LEO  

Pata Dira ya Dunia kupitia Star TV

By Mhariri - Aug 24, 2012


IDHAA ya Kiswahili ya BBC imezindua kipindi cha habari cha Dira ya Dunia hapa nchini ambacho kitarushwa moja kwa moja kutoka Londonkupitia Kituo cha Televisheni cha Star(Star TV)
Kipindi hicho cha nusu saa kitakuwa cha kwanza duniani kutangazwa kwa Kiswahili kupitia televisheni ya Star Tv hapa nchini.

Mhariri wa BBC Idhaa ya Kiswahili, Ali Saleh alisema kipindi hicho cha nusu saa kitaanza kurushwa rasmi Agosti 27,mwaka huu kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa saa 3 usiku kupitia  Star Tv.

Saleh alisema kipindi hicho kitatoa chachu katika matangazo ya Star TV kwa kuwaletea watazamaji wa habari za kiwango cha juu kutoka katika kitovu cha habari za dunia cha BBC-Global News. “Uzinduzi wa Dira ya Dunia kupitia TV, ni kwenda na mabadiliko tunayoyashuhudia ya jinsi watu wanavyofuatilia habari barani Afrika, na pia mahitaji ya mashabiki wa BBC Idhaa ya Kiswahili,”alisema Saleh na kuongeza.

“Dira ya Dunia itawaletea watazamaji taswira na uchambuzi yakinifu kutoka kwa waandishi wa habari waliotapakaa katika nchi 48 barani Afrika, na hivyo kuleta picha halisi ya bara zima kwa watazamaji wanaozungumza Kiswahili”.
Huyu ndiye Salimu Kikeke, mtangazaji wa kipindi hicho

Alisema Dira ya Dunia itatoa taswira halisi ya Afrika, tofauti na jinsi ambavyo bara hili limekuwa likiripotiwa kwa miaka mingi. Kipindi chetu kitakuwa kinashirikisha watazamaji, na pia kuzigatia misingi ya BBC ya muda mrefu ya uhuru, uhakika na bila upendeleo.

Mpaka sasa BBC ina mashabiki 239 milioni kwa wiki duniani kote katika huduma zake za habari za kimataifa ikiwemo BBC World Service, BBC World News TV na bbc.com/news.

BBC Idhaa ya Kiswahili ni sehemu ya BBC Idhaa ya Dunia (BBC World Service), ambao ni watangazaji wa kimataifa wanaotoa huduma ya matangazo kwa lugha mbalimbali kupitia redio, TV na kwenye wavuti na pia kupitia vifaa vitumiavyo visiwaya. 

CHANZO: Mwananchi

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII