Jinsi ya kutambua akaunti za uongo za facebook na kuwa salama
By Mhariri - Aug 5, 2012

Mtu anaweza kujiuliza swali iweje iwe rahisi kiasi hiki kusumbuliwa au kukutwa na uharifu wa mtandaoni kupitia akaunti yako ya facebook ambayo umeifungua kwa nia njema kabisa. Kwa faida yako unashauriwa kufuata maelekezo yaliyopendekezwa kama njia moja wapo ya kujiweka salama. Maelezo haya yatakuongoza kujua namna ya kuzigundua akaunti za uongo na kujiepusha na watu wa jinsi hiyo. Pamoja na hayo bado unaweza ukakutana na akaunti ambayo ni halisi na mtumiaji wake anafahamika, lakini sio kigezo cha kujiaminisha asilimia 100 juu ya kile unachokifanya ukiwa mtandaoni.
Kama ushauri tu, wakati wewe unafurahia huduma zipatikanazo katika mitandao ya kijamii kuna watu usiku na mchana hawalali wanawaza jinsi gani waweze kunufaika na mtandao huo huo ambao wewe unautumia. Kama unakumbuka vizuri kuna tukio lilifedhehesha watu humu facebook mwezi wa Mei na kufanya baadhi yetu akaunti zao zipotee kabisa.
Tukio lilihusu picha ya video ya Rihana, ilikuja kama link fulani, cha kushangaza kila aliyeigusa tu alionekana kuwa ndiye aliyepost picha hiyo na kutapakaa kwa marafiki zake ikiwashawishi nao kuangalia. Katika hali ya kawaida unapoona post imekuja kwa jina la rafiki yako wa karibu sana lazima tu utaiangalia. Nilipatwa na mkasa huo lakini kwa kuwa binafsi najiita BA Facebook, niliweza kukabiliana nayo.
Kuhusu usalama wa akaunti yako:
MAELEKEZO NA MICHORO YA KUREKEBISHA TAARIFA ZA USALAMA KWA AJILI YA AKAUNTI YAKO YA FACEBOOK YATAKUIJIA HIVI PUNDE. USIKAE MBALI NA MAGANGA MEDIA.
KAMA UNA SWALI LOLOTE LIANDIKE KWENYE SEHEMU YA MAONI CHINI YA HABARI HII ILI YAWEZE KUJIBIWA MOJA KWA MOJA AU KATIKA MAKALA ZINGINE ZITAKAZOFUATA. MAONI YAKO NI MSINGI WA MABORESHO YA HUDUMA ZETU.


CLICK HERE TO READ IT.
Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS
ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII