HABARI MPYA LEO  

AJIRA ZA UALIMU AWAMU YA PILI : Wizara ya Elimu

By Maganga Media - Mar 18, 2012

AJIRA MPYA YA WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI WENYE ELIMU YA SHAHADA NA STASHAHADA MWAKA 2011/12 

Kwa waombaji wote walioomba nafasi za kazi / ajira ya Ualimu Wizara 
ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ambao majina yao yametangazwa katika tovuti za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Ofisi ya Waziri Mkuu- TAMISEMI, Wanatakiwa kuripoti tarehe 19 Machi 2012  kwenye Ofisi za Wakurugenzi wa Halmashauri husika kwa ajili ya  kupangiwa Vituo vya kazi. Kila mwalimu anatakiwa kwenda na VYETI vyake halisi kwenye Halmashauri alikopangwa. HAKUNA MABADILIKO YATAKAYOFANYWA. Mwalimu ambaye hataripoti ifikapo tarehe 25 Machi 2012 atapoteza nafasi hiyo. 
CHAGUA KUNDI HAPA:    SHAHADA                                 STASHAHADA

NB:
WALIMU WALIOKWISHA PANGWA AWAMU YA  KWANZA AMBAO WANAOMBA  KUPANGWA UPYA, MAOMBI HAYO HAYAKUKUBALIWA, WANATAKIWA WAKARIPOTI MARA MOJA KATIKA VITUO WALIVYOPANGIWA AWALI. AIDHA WAKURUGENZI WA HALMASHAURI HUSIKA WAWAPOKEE NA KUWAPANGIA VITUO VYA KAZI.

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII