HABARI MPYA LEO  

Ocampo amtaka Ntaganda

By Maganga Media - Mar 18, 2012

Luis Moreno Ocampo anasema kua Bosco Ntanganda lazima akamatwe na ahamishiwe kwenye korokoro za ICC mara moja.
Gen.Bosco Ntaganda
Gen.Bosco Ntaganda

Yeye anatakiwa kwa kuwasajili, kuorodhesha na kuwatumiaaskari watoto wakati wa mapigano ya wenyewe kwa wenyewe huko Ituri.
Bw.Ocampo anasema kua upande wa mashtaka unapanga kuongezea mashtaka mengine ya mauwaji na ubakaji kwenye waranti ya kumkamata.
Kwa wakati huu Bw.Ntanganda yuko katika Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo kama Jenerali.
Mwanasheria huyo amesema kua ulimwengu hauwezi kukaa kitako huku washukiwa wa uhalifu wakiendelea kuishi huru miongoni mwa umma.
Bw.Ocampo ana mipango ya kumtembelea Rais Kabila mwezi ujao kujadili jinsi ya kumkamata Bosco Ntaganda na kumfikisha huko The Hague.

http://maganga-resources.blogspot.com

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII