HABARI MPYA LEO  

Mwanafunzi aliyeandika bongo fleva kwenye mtihani wa kidato cha nne ajitokeza na kueleza nia yake!

By Unknown - Jul 13, 2012

Julius a.k.a Elinaja. FROM MILLARD AYO

Yule mwanafunzi aliyetangazwa na baraza la mitihani Tanzania (NECTA) February 8 2012 wakati baraza la mitihani lilipotangaza matokeo ya kidato cha nne kuwa aliamua kuandika mistari ya bongo fleva kwenye sehemu ya kujibia maswali amejitokeza na kueleza nia yake. Amesema ameona muda unaenda na yeye hajatimiza nia yake, alichokusudia hakijajulikana hivyo ni bora amejitokeza.

HIKI NDICHO ALICHOANDIKA KWENYE MTIHANI WAKE

“nashukuru sana wanaosahihisha mitihani hii ya shule yangu, nitakapofeli naendelea na fani yangu ya bongofleva, Majita wangu wako levo za juu na sio East Zuu, kukosa ni kawaida kwa binadamu” hiyo ilikua ni swali namba 6 na 7

kwenye swali la 11 kwenye moja ya mitihani yake aliandika mistari ya bongofleva kwamba “acha utani my girl, unakuja nyumbani umezizi mwenzako huku naona sijiwezi, kazi hiyo ya kuzizi nakwambia ukweli mwanzo ulikua mzuri lakini mwisho ukawa mbaya”

JINA LAKE KAMILI

Baada ya hayo matokeo watu wengi sana walitamani kumfahamu huyu mwanafunzi, Jina lake la kuzaliwa ni Julius lakini la kisanii ni Elinaja, na ametoa sababu 5 za kwa nini aliamua kuandika hiyo mistari ya bongo fleva kwenye mitihani yake ya kumaliza kidato cha nne.

SABABU TANO (5) ZA KUANDIKA BONGOFREVA KWENYE MAJIBU YA MTIHANI:

  1. Kutaka kutuma ujumbe kwa watu wanaosimamia Elimu kwa ujumla,
  2. Kutaka kusaidia watu wanaoteseka mtaani ambao wanaishi maisha magumu kwa sababu tu ya kushindwa kwendana na system ya elimu iliyopo ambayo ukishindwa kwenda nayo sawa umefeli, tulivyoumbwa kuna mtu anaweza akawa anashindwa kitu flani lakini ni mzuri kwenye kitu kingine sasa mfumo uliopo hautoi nafasi kwa wasioweza hiyo system,
  3. Sababu ya tatu ni kutokana na utaratibu wa usaishaji wa mitihani kwa sababu sijui kama kuna mwanafunzi yeyote aliewahi kufanya mtihani wake wa mwisho alafu mtihani wake ukarudishwa ili kuona wapi alipokosa na wapi alipopata”
  4. Sababu ya nne ni kuhusu wazazi kutambua uwezo wa watoto wao toka wakiwa wadogo kipi wanaweza kipi hawawezi ili kuokoa muda na pesa,
  5. Sababu ya tano ni kwa serikali ijaribu kuweka shule za vipaji toka mwanafunzi akiwa mdogo kabisa, leo hii kuna mtu amepata degree pale chuo kikuu kasoma miaka mitatu na kupewa degree ya sanaa lakini hawezi kukuonyesha cheti hata kimoja kwamba alikua na elimu ya awali ya hiyo degree, huwezi kuniambia una degree wakati hukupata elimu ya msingi ya ulichosomea”

“Kwa namna moja au nyingine sidhani kama nimefanikiwa kwa sababu nilichofanya watu walikichukulia tofauti sikufanikiwa ndio maana nimeamua kujitokeza kumalizia kazi ambayo niliianza kuifanya kule kwa sababu nafsi yangu ilikua inanisuta, ila kwa sasa watu watakua wameelewa na ninaweza kuwasaidia watu wengine” – Julius (Elinaja)

From: millardayo.com

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII