HABARI MPYA LEO  

PESA ZA RADA KUNUNULIA VITABU

By Maganga Media - Mar 16, 2012

Moja ya ndege za BAE
Kampuni ya kuuza vifaa vya kijeshi ya BAE Systems itatoa takriban £29.5m kwa miradi ya elimu nchini Tanzania kufuatia makubaliano na Taasisi ya Kupambana na ufisadi ya Uingereza (SFO). BAE ilipigwa faini ya £500,000 mwaka 2010 kwa kushindwa kutunza rekodi zake za malipo iliyofanya kwa mshauri wake.
Malipo hayo yalitolewa kununua rada ya kijeshi kwa Tanzania kwa gharama ya £28m. Kampuni hiyo ya BAE sasa imethibitisha makubaliano ambayo yatatumika kusaidia watanzania kama ilivyoafikiwa
.
Itanunua vitabu vya kiada kwa shule 16,000 vya masomo muhimu ya Kiswahli, Kiingereza, Hisabati na Sayansi. Fedha hizo pia zitatumika kuwapatia miongozo walimu na mwongozo wa muhtasari wa masomo kwa waalimu wote 175,000 wa shule za msingi, na muhtasari yenyewe, kampuni hiyo ya ulinzi imesema.


Taasisi ya SFO ilisema makubaliano hayo yalikuwa ya kwanza na ya aina yake, lakini ilikosolewa na jaji aliyetoa uamuzi wake kwa kampuni hiyo miaka miwili iliyopita. "Makubaliano haya ni ya kwanza kwa SFO ambayo iliratibu kutumia mfumo wa sheria za Uingereza,’ mkurugenzi wa SFO Richard Alderman alisema. 'hatma ya jambo lenyewe' "Tumefurahi kuwa hatimaye tumefikia mahali tunaweza kutoa malipo kwa serikali yaTanzaniana kufikia tamati ya suala hili." BAE ilisema.

BAE iliafikiana na SFO mpango huo mwaka 2010. Ilikubali kulipa faini ya na gharama ya £225,000 kwa SFO – na faini ilikokotolewa kutoka £30m iliyotoa kwa watanzania kumaliza kesi hiyo.

Wakati huo jaji wa mahakama ya Southwark Crown alikosoa makubaliano hayo kati ya SFO na BAE. "Muundo wa makubaliano hayo unaweka shinikizo la kimaadili kwa mahakama kuifanya faini hiyo iwe kwenye kiwango cha chini kwa ajili ya maandalizi ya juu. " alisema Justice Bean, aliyeongeza kuwa alikuwa kwenye shinikizo la kuiweka faini ya mahakama kuwa ya chini.

Pia alikosoa sehemu nyingine ya makubaliano ambayo alisema yalimpa mjumbe yeyote wa kampuni ya BAE Systems "kinga kwa makosa yote yaliyofanywa nyuma yawe yamewekwa wazi au la". Kampuni hiyo ililipa £7.7m kwa kampuni mbili zinazomilikiwa na mfanyabiashara Shailesh Vithlani kabla hata ya kushinda zabuni yenyewe ya kununua rada.

http://maganga-resources.blogspot.com

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII