HABARI MPYA LEO  











Kesi ya mauaji ya marehemu Steven Kanumba inayomkabili movie star wa Tanzania Elizabeth Michael (Lulu) imeendelea kutajwa katika mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam huku suala la umri wa mshitakiwa huyo likiendelea kuwekwa kiporo.

Mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu AUGUSTINA MMBANDO, Wakili wa Serikali KENNETH SEKWAO amesema upelelezi bado haujakamilika na kwa sasa ipo katika hatua ya kutajwa.

Mapema baada ya LULU kufunguliwa mashitaka ya mauaji ya msanii mwenzake STEVEN KANUMBA April mwaka huu, mawakili wanaomtetea waliwasilisha hoja ya kupinga umri wa mshitakiwa huyo na kutaka achukuliwe kama mkosaji mtoto kutokana na umri wake kuwa chini ya miaka 18 hali iliyolazimu suala hilo kupelekwa Mahakama Kuu ya Tanzania iliyoamua kulirejesha jambo hilo kwenye mahakama ya Kisutu.

Pamoja na kurejeshwa kwa suala hilo katika mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu kumekuwa na ukimya wa muda sasa, kesi ya LULU imeahirishwa mpaka Disemba 17 mwaka huu ambapo itakwenda kwaajili ya kutajwa.
Maelfu ya Walibya wamefanya mhadhara katika mji wa Benghazi, mashariki mwa Libya, kuunga mkono demokrasi na kuwapinga wapiganaji wa Kiislamu.
Maandamano ya kupinga wapiganaji mjini Benghazi
Waandamanaji waliisihi serikali ya Libya iyapige marufuku makundi ya wapiganaji ambao wamekataa kukabidhi silaha zao tangu vita dhidi ya Kanali Gaddafi mwaka jana. Waandamanaji wanataka serikali izidishe jeshi na polisi, na walimsifu balozi wa Marekani aliyeuliwa mjini humo juma lilopita. Waliimba wakati wakiandamana kuelekea medani kuu ya Benghazi.

Muandamanaji mmoja, Faisla al-Naas, alieleza sababu zao: "Sisi tunaandamana kupinga kundi lenye silaha ambalo halidhibitiwi na serikali. Wapiganaji hawa wanafaa kujiunga na serikali ili watu wakae kwa salama.
Nchi yetu imekuwa na mtafaruku."

Maandamano mengine ya kuunga mkono wapiganaji yalikuwa madogo sana.
DUNIA haikaukiwi matukio ya kustaajabisha, kwa hakika huu ni ulimwengu maridhawa na hawakukosea walionena kwamba dunia hadaa ulimwengu shujaa.
 
Stori ya kusikitisha, inatokea nchini Marekani ambako kijana Justin Street, amepoteza maisha akiwa kwenye jaribio la kuongeza ukubwa wa nyeti yake.


Habari kamili ipo hivi; Justin, 22, akiwa baba wa watoto wawili alikwenda kwa mwanamama Kasia Rivera ,35, aliyejitangaza kuwa ni mtaalamu wa tiba za kuongeza ukubwa wa nyeti za kiume.


Kasia aliweka matangazo barabarani kuwa anayo tiba ya kuongeza ukubwa wa nyeti za kiume, hivyo kumfanya Justin ahamasike kwenda kupata dawa hiyo ili kujiongezea ushababi. 


Wanasema tamaa mbele mauti nyuma, ndivyo ilivyotokea kwa Justin, kwani baada ya kuomba dawa ya kuongeza ukubwa wa maumbile yake ya kiume, alidungwa sindano yenye madini ya silikoni.


Madini hayo, alidungwa kwenye nyeti yenyewe na baada ya muda mfupi, hali ya afya yake ilibadilika kuwa mbaya, alizorota na siku iliyofuata alifariki dunia.


Kutokana na tatizo hilo, Kasia alifikishwa mahakamani kwa kesi ya mauaji akituhumiwa kufungua zahanati bubu ndani ya nyumba yake iliyopo New Jersey, vilevile kutoa tiba za kiafya wakati hana taaluma hiyo wala leseni ya kuendesha kazi hiyo ya utoaji huduma za afya.


Kasia alipandishwa kizimbani wiki iliyopita, uchunguzi wa maiti umethibitisha kwamba Justin alifikwa na mauti baada ya madini ya silikoni aliyodungwa kwa sindano kuziba njia za mishipa ya damu.


Mmoja wa madaktari waliomfanyia uchunguzi Justin alisema kuwa hii ni mara ya kwanza kusikia silikoni inayotumika kuongeza ukubwa wa matiti ya wanawake imetumika kwenye kuongeza ukubwa wa uume.Kasia, amekana kuhusika na mauaji hayo.


WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amewavua madaraka wakurugenzi sita wa Halmashauri za Wilaya kwa kushindwa kusimamia rasilimali watu, fedha na kutowajibika.

Kutokana na hatua hiyo, Waziri Mkuu Pinda amewateua watu sita kukaimu nafasi hizo na wakurugenzi wapya 14 huku akiwahamisha wakurugenzi 27 kutoka katika vituo vyao vya kazi kwa sababu mbalimbali.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Hawa Ghasia, alisema wakurugenzi hao walivuliwa madaraka kwa kushindwa kusimamia rasilimali watu na fedha, kusababisha halmashauri kupata hati chafu na uzembe.

Aliwataja wakurugenzi hao waliovuliwa madaraka kuwa ni Willy Njau (Mwanga), Mpangalukela Tatala (Geita), Theonest Nyamhanga (Kishapu), Eden Munisi (Morogoro), Mhando Senyagwa (Kyela) na Nicholaus Kileka (Ngorongoro).

Pia alisema Serikali haitasita kuchukua hatua pale inapobidi ili kuboresha utendaji, na kwamba wengine tayari wana kesi na si busara kuwe na mtu anayekaimu zaidi ya miaka mitatu.

Pia alisema hatua za kinidhamu bado zinaendelea na kwamba baadhi ya wakurugenzi hao tayari wamewafikisha kwenye Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa ajili ya hatua zaidi.

Waziri huyo aliwataja wakurugenzi wapya walioteuliwa kujaza nafasi hizo kuwa ni Abdalah Kidwanka (Geita), Rutius Bilakwata (Kishapu), Naomi Nko (Magu ), Abdalah Mfaume (Kyela), Twalib Mbasha (Monduli), Henry Ruyagu (Urambo), Adam Mgoyi (Mbarali) na Estomih Chang’a (Mpanda).

Wamo pia Leti Shuma (Mwanga), Mohamed Maje (Namtumbo) Fulgency Mponji (Moshi), Robert Nehata (Tunduru), Isabela Chilumba (Kahama), Fikiri Malembeka (Sengerema), Paul Malala (Njombe) na Nasib Mbaga (Biharamulo).

Wakurugenzi wanaohamishwa ili kujaza vituo wazi ni Bibie Mnyamagola (Kongwa), Daudi Mayeji (Kilindi), Protace Magayane (Nkasi), Saada Mwaruka (Mkuranga), Sipora Liana(Tabora Manispaa), Hadija Makuwani (Wilaya ya Tabora), Doroth Rwiza (Kasulu).

Wengine ni Kelvin Makonda (Manispaa ya Lindi), Pudenciana Kisaka (Iringa), Tina Sekambo (Makambako), Beatrice Dominick (Masasi), Gladyness Ndyamvuye (Bukoba), Nathan Mshana (Ngorongoro), Cornel Ngudungi (Ngara), Mohamed Mkupete (Mtwara Manispaa), Dk Koroine Ole Kuney (Misungwi).

Wamo pia Ephraem Ole Nguyaine (Rorya), Goody Pamba (Igunga), Fidelis Lumato (Ludewa), Athuman (Tarime) na Ahmad Sawa (Musoma Manispaa).

Waliohamishwa kwenda kwenye halmashauri mpya ni Magreth Nakainga (Geita), Eliza Bwana (Bariadi), Zuberi Mbyana, Ilemela Manispaa (Biharamulo), Mohamed Nanyanje (Masasi), Erica Musika (Kahama), Imelda Ishuza (Busokelo).

Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz/habari

Juzi malori 30 yaliyokuwa yamejaa sarafu (ama kunogesha zaidi chenchi) za senti tano tano, yaliwasili kwenye makao makuu ya Apple, jimboni California, Marekani.

Awali, walinzi wanaolinda makao hayo makuu walidhani malori hayo yamepotea njia, lakini dakika chache baadaye, Tim Cook (CEO wa Apple) alipokea simu kutoka kwa CEO wa Samsung Lee Kun-hee, akimueleza kuwa wamewalipa faini yao ya dola bilioni 1, kutokana hukumu dhidi ya kampuni hiyo ya Kikorea.
Tim Cook
Kitu cha kuchekesha zaidi ni kuwa nyaraka iliyosainiwa haioneshi njia moja ya kulipa faini hiyo, hivyo Samsung ilikuwa na haki ya kuwapelekea faini hiyo watengenezaji hao wa simu za iPhone vyovyote wanavyotaka.

Lee Kun-hee
Mchezo huu mchafu na wa kijanja utawaumiza kichwa wakurugenzi wa Apple kwakuwa itabidi iwachukue muda mrefu kuhesabu fedha zote ili kuhakikisha kama zimetimia na kujaribu kuzipeleka benki ambako hawajui kama zitakubalika.

Mwenyekiti wa Samsung Electronics Lee Kun-hee, amewaambia waandishi wa habari kuwa kama Apple wanataka kucheza mchezo mchafu na wao pia wanaujua. Undava undava na kama noma iwe noma tu!
Wendesha mashtaka wa serikali nchini Afrika Kusini wanasema kuwa wanajianda kuwafungulia mashtaka ya mauaji wachimba migodi wa mgodi wa Marikana.  Ripoti zinasema pia, wachimba migodi hao, wanakabiliwa na mashtaka mengine ikiwemo jaribio la mauaji ya wachimba migodi thelathini na wanne ambao waliuawa kwa kupigwa risasi na polisi.

Msemaji wa ofisi ya kiongozi wa mashtaka nchini humo, amesema ikiwa watu, ambao baadhi yao wamejihami wakiwakabili polisi na kutokee mauaji, wale watakaoshikwa na polisi watafunguliwa mashtaka ya mauaji, bila kujali wale waliofyatua risasi.

Polisi waliwapiga risasi wachimba migodi hao kufuatia ghasia na maandamano kuhusu mishahara.
Maafisa wawili wa polisi waliuawa kwenye machafuko hayo.