HABARI MPYA LEO  

Mkenya avunja rekodi Olympic

By Mhariri - Aug 10, 2012


Mkenya David Lekuta Rudisha ameibuka kuwa mwanariadha wa kwanza kuandikisha rekodi mpya kwenye mashindano ya riadha katika michezo ya Olimpiki, inayoendelea jijini London Uingereza na kisha kushinda medali ya dhahabu katika mbio za mita mia mbili.

Akiwa anashiriki fainali ya michezo ya Olimpiki kwa mara kwanza, Rudisha mwenye umri wa miaka 23 alinyakuwa ushindi huo kwa kuwa mtu wa kwanza kukimbia umbali wa mita mia nane kunako dakika 1, sekunde 40 nukta 91.

Mwariadha wa Botswana Nijel Amos, umri 18, alinyakuwa medali ya fedha huku chipukizi mwingine kutoka Kenya Timothy Kitum, akiridhika na medali ya shaba.

Mwingireza Andrew Osagie alimaliza katika nafasi ya nane lakini akaweza kuandikisha muda bora wa dakika 1:43.77.

Rudisha ambaye ni bingwa wa dunia aliongoza katika mbio hizo tangu mwanzo hadi mwisho na kuwaacha wanariadha wenzake kwa tofauti ya sekunde 49.28. Kisha akafyatuka katika hatua za mwisho mwisho na kuivunja rekodi yake mwenyewe.

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII