HABARI MPYA LEO  

Blatter: niko tayari kumfunga Bale

By Unknown - Jul 26, 2012

Rais wa FIFA Sepp Blatter amesema kua mchezaji wa klabu ya Tottenham Gareth Bale anaweza kukabiliwa na vikwazo kwa kuichezea klabu yake wakati wa mashindano ya Olympic ikiwa chama cha FA kitawasilisha malalamiko yake kua mchezaji huyo ameweza kuichezea klabu yake na kukataa kuichezea Timu ya Uingereza(GB).

Bale alifunga bao la Spurs katika mchuano uliomalizika kwa sare ya 1-1 dhidi ya LA Galaxy katika ziara ya klabu hiyo nchini Marekani. Bale alijiondoa kutoka timu ya GB inayojumuisha wachezaji kutoka kote Uingereza, Wales na Scotland kwa kudai majeruhi.
Gareth Bale
Chama cha mpira cha FA na shirikisho la Olimpiki hayajatoa tamko lolote kuhusu kujitokeza kwa mchezaji huyo lakini Bw.Blatter anasema ikiwa shirika hilo litawasilisha malalamiko yao kwetu basi mchezaji huyo atawekewa vikwazo wakati wa Olimpiki.

Hata hivyo klabu ya Spurs inaweza kujitetea kwa kusema kua mchezaji huyo Bale alipata nafuu katika siku chache zilizopita, na hivyuo kutetea uwamuzi wa mchezaji huyo kujiondoa kwenye kikosi cha Blatter cha GB.
Bale alicheza kwa mda wa dakika 74 za mechi hio dhidi ya Galaxy, na baadaye Villas-Boas akasema kua "Gareth bado ni kijana na ana nguvu za kupindukia kwa hiyo aliweza kuongeza juhudi zake.

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII