HABARI MPYA LEO  

Wanafunzi bora kidato cha sita 2012

By Maganga Media - May 2, 2012

Dk Ndalichako alisema mwaka huu walishindanisha ubora wa watahiniwa kwa kuzingatia aina ya masomo wanayochukua.

Katika kundi la wanafunzi bora kwenye Sayansi lililoongoza na Faith, aliyefuata ni Zawadi Mdoe (Feza), Belnadino Mgimba (Minaki), Jamal Juma (Feza) na Imaculate Mosha (Marian).

Watano waliofanya vizuri katika masomo ya Biashara wakiongozwa na Alex ni Ephraim Tumwidike (St Joseph's Cathedral), Vaileth Mussa (Weruweru), Seleman Manyiwa (Kibaha) na Hussein Issa (Azania).

Katika masomo ya Lugha na Sayansi ya Jamii aliyemfuata Faridi ni Jema Rwihura (Weruweru), Mariam Hincha (Weruweru), Neema Mbandwa (Igawilo) na Hemed Hussein (Tosamaganga).

Wasichana watano bora kwa masomo ya Sayansi, wote wametoka Marian ambao ni Faith Immaculate Mosha, Rachel Sigwejo, Mary Kiangi na Nashival Kivuyo.

Wavulana bora katika Sayansi ni Zawadi, Belnadino, Jamal Juma (Feza), Gwamaka Njobelo na Nickson Mwamsojo; wote kutoka Mzumbe.

Wasichana waliofanya vizuri zaidi katika masomo ya Biashara, nafasi ya kwanza hadi ya nne ilichukuliwa na wanafunzi wa Weruweru, ambao ni Vaileth, Gloria Murro, Stella Richard na Helen Komba. Nafasi ya tano ilichukuliwa na Veronica Sauli wa St. Antony.

Wavulana waliofanya vizuri katika masomo ya biashara ni Alex, Aphraim, Suleiman, Hussein na Ally Katala wa Azania.

Wasichana watano waliofanya vizuri masomo ya Lugha na Sayansi ya Jamii ni Jema, Mariam, Neema Mbandwa (Igawila), Angel Ruhumbika (Loreto) na Jaquline Chambua (St. Mary's Mazinde Juu).

Wavulana waliofanya vizuri katika masomo ya Lugha na Sayansi ya Jamii ni Faridi, Hemed, Elibaraka Mmari (Lyamongo) na Salvatory Kessy (Majengo).

Matokeo yaliyozuiwa

Dk Ndalichako alisema watahiniwa sita, watatu kati yao wakiwa wa kujitegemea walifutiwa matokeo yao baada ya kubainika kuwa walifanya udanganyifu.

Alisema pia Necta imezuia matokeo ya watahiniwa 51 ambao kwa mujibu wa kumbukumbu zao hawajalipa ada ya mtihani.Dk Ndalichako alisema matokeo yao yatatolewa na Necta pindi watakapokamilisha taratibu za malipo hayo.

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII