HABARI MPYA LEO  

MADAKTARI WAMPONGEZA RAIS

By Maganga Media - May 5, 2012

Aliyekuwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hadji Mponda

CHAMA cha Madaktari  Tanzania (Mat) kimeeleza kufurahishwa na hatua ya Rais Jakaya Kikwete kuwaondoa aliyekuwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hadji Mponda na Naibu wake, Dk Lucy Nkya, kuwa ametekeleza madai yao.

Pia, chama hicho kimesema kimefurahishwa na uteuzi wa Dk Hussein Mwinyi kuwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii kwa sababu, ni mtendaji anayeaminika.

Katibu Mkuu wa Mat, Dk Rodrick Kabangila, alisema madaktari wamefurahi kuondolewa kwa mawaziri waliokuwapo kwa sababu walikuwa kikwazo kwenye utekelezaji wa madai yao.

“Kwa sasa tuna imani na Serikali, madai yetu na hata yale tunayojadili baina yetu na Serikali yatatekelezwa, tunasema hivyo kwa sababu kama wangeendelea kubaki mawaziri wa awali utekelezaji wake ungekuwa na mashaka,” alisema Dk Kabangila.

Kabangila alisema mawaziri hao walikuwa wagumu wa kutekeleza madai yao na wakati mwingine, walioonekana kuwadharau hali iliyosababisha waingie kwenye mgomo.

“Dk Mwinyi tunamfahamu, wakati madaktari tulipogoma mwaka 2004/05 alikuwa Naibu waziri alikuja kutusikiliza, yapo mambo alichukua hatua kwa wakati,” alisema Dk Kabangila na kuongeza:

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII