BIASHARA huria imezua mengi. Hali kadhalika Sayansi na Tekenolojia nayo, imeleta mengi. Katika kuwaondolea kero wanawake wenye matiti yaliyosinyaa hapa nchini, wataalamu kutoka China wameanza kutoa huduma ya kunyanyua matiti hayo kwa kutumia mashine maalumu.
Wachina wamejipatia umaarufu katika kuleta bidhaa mbalimbali hapa nchini, zikiwamo za kuongeza nguvu za kiume, kupunguza uzito, kuotesha nywele, kujichubua (kumfanya mtu mweusi awe mweupe), kuongeza makalio nk.
Huduma hiyo ya kusimamisha matiti yaliyolala, imeanza kutolewa katika Saluni ya Blue Palace, iliyopo nyuma ya Shule ya Mapambano, Sinza jijini Dar es Salaam.
Haikuwa rahisi kuweza kuamini kuwa vitu kama hivi vinaweza kupatikana Tanzania. Mwananchi Jumapili lilifunga safari mpaka kwenye saluni hiyo inayomilikiwa na Sarafina Mtweve, kujionea jinsi teknolojia hiyo inavyofanya kazi.
Mbali na meneja wa saluni hiyo, Trust Mwembe, pia alikuwepo mtaalamu kutoka China aitwaye, Ciisy Pang, ni binti wa miaka 23 tu, lakini anasema kwa miaka minne amefanya kazi hiyo na kuwasaidia wanawake mbalimbali waliokuwa wakikerwa na matiti yaliyolegea au kuanguka.
Pang na kundi lake wanatoa huduma hii kwa gharama ya Sh150,000 kwa kuanzia, ingawa wanahisi gharama hizo zitapanda katika siku chache zijazo.
Jinsi matiti yanavyosimamishwa
![]() |
| Moja ya ndege za BAE |
Malipo hayo yalitolewa kununua rada ya kijeshi kwa Tanzania kwa gharama ya £28m. Kampuni hiyo ya BAE sasa imethibitisha makubaliano ambayo yatatumika kusaidia watanzania kama ilivyoafikiwa
.
Itanunua vitabu vya kiada kwa shule 16,000 vya masomo muhimu ya Kiswahli, Kiingereza, Hisabati na Sayansi. Fedha hizo pia zitatumika kuwapatia miongozo walimu na mwongozo wa muhtasari wa masomo kwa waalimu wote 175,000 wa shule za msingi, na muhtasari yenyewe, kampuni hiyo ya ulinzi imesema.
Taasisi ya SFO ilisema makubaliano hayo yalikuwa ya kwanza na ya aina yake, lakini ilikosolewa na jaji aliyetoa uamuzi wake kwa kampuni hiyo miaka miwili iliyopita. "Makubaliano haya ni ya kwanza kwa SFO ambayo iliratibu kutumia mfumo wa sheria za Uingereza,’ mkurugenzi wa SFO Richard Alderman alisema. 'hatma ya jambo lenyewe' "Tumefurahi kuwa hatimaye tumefikia mahali tunaweza kutoa malipo kwa serikali yaTanzaniana kufikia tamati ya suala hili." BAE ilisema.
BAE iliafikiana na SFO mpango huo mwaka 2010. Ilikubali kulipa faini ya na gharama ya £225,000 kwa SFO – na faini ilikokotolewa kutoka £30m iliyotoa kwa watanzania kumaliza kesi hiyo.
Wakati huo jaji wa mahakama ya Southwark Crown alikosoa makubaliano hayo kati ya SFO na BAE. "Muundo wa makubaliano hayo unaweka shinikizo la kimaadili kwa mahakama kuifanya faini hiyo iwe kwenye kiwango cha chini kwa ajili ya maandalizi ya juu. " alisema Justice Bean, aliyeongeza kuwa alikuwa kwenye shinikizo la kuiweka faini ya mahakama kuwa ya chini.
Pia alikosoa sehemu nyingine ya makubaliano ambayo alisema yalimpa mjumbe yeyote wa kampuni ya BAE Systems "kinga kwa makosa yote yaliyofanywa nyuma yawe yamewekwa wazi au la". Kampuni hiyo ililipa £7.7m kwa kampuni mbili zinazomilikiwa na mfanyabiashara Shailesh Vithlani kabla hata ya kushinda zabuni yenyewe ya kununua rada.




Vijembe na tambo vyatamalaki























