HABARI MPYA LEO  

Khartoum Waandamana kupinga serikali kubana matumizi

By Unknown - Jun 24, 2012

Waandamanaji mjini Khartoum, Sudan, wametumia matairi waliyoyaasha moto na mawe kuwazuwia polisi waliojaribu kuzima maandamano dhidi ya serikali kupinga hatua ya serikali ya kubana matumizi.
Moshi wa matayri yaliyochomwa kwenye maandamano mjini Khartoum

Maandamano hayo awali yaliongozwa na wanafunzi, lakini inaarifiwa na wananchi wengine nao wamejiunga nayo.

Polisi wa Sudan wameamrishwa kuchukua hatua haraka kumaliza fujo hizo.

Maandamano hayo yaliyoanza tarehe 16 Juni, yalichochewa na hatua za serikali za kupambana na msukosuko wa kiuchumi, uliotokana na Sudan Kusini kusimamisha kusafirisha mafuta yake kwa kupitia Sudan.

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII