HABARI MPYA LEO  

Waziri mkuu, atangaza wakuu wa wilaya

By Maganga Media - May 9, 2012



Waziri Mkuu Mheshimiwa MIZENGO PINDA ametangaza Wakuu wapya wa Wilaya huku Wakuu wa Wilaya 51wa zamani akiwaacha kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ya kustaafu kazi.

Akitangaza Wakuu hao wapya wa Wilaya mbele ya Wahariri wa vyombo vya habari nchini, Waziri Mkuu amesema kati ya Wakuu hao wa Wilaya 133 walioteuliwa wapya ni Sabini wakiwemo Waandishi wa habari Sita.

Kulingana na Waziri Mkuu kabla ya kutangazwa kwa Wilaya mpya kulikuwa na Wakuu wa Wilaya 114 ambapo kati ya Wakuu hao wa Wilaya wa Zamani 63 wamebaki katika uteuzi wa leo na 51 wameachishwa kazi.

mkuu wa wilaya mkoa wa Mbeya aliyetangaza kujiuzulu atemwa rasmi

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII