Maelfu ya Walibya wamefanya
mhadhara katika mji wa Benghazi, mashariki mwa Libya, kuunga mkono
demokrasi na kuwapinga wapiganaji wa Kiislamu.

Muandamanaji mmoja, Faisla al-Naas, alieleza sababu zao: "Sisi tunaandamana kupinga kundi lenye silaha ambalo halidhibitiwi na serikali. Wapiganaji hawa wanafaa kujiunga na serikali ili watu wakae kwa salama.
Nchi yetu imekuwa na mtafaruku."
Maandamano mengine ya kuunga mkono wapiganaji yalikuwa madogo sana.