HABARI MPYA LEO  

Matukio Ya Uokoaji Ajali Ya Meli Zanzibar

By Unknown - Jul 19, 2012


Waokoaji wakiwa kazini kwenye Meli ya Kilimanjaro


Muokoaji akiwa na maiti

Waokoaji wakiwa na majeruhi kwenye moja ya Boti za uokoaji.

Majeruhi wa wakipatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Mnazi Mmoja

MV KMKM ikiwa kazini

Raia wa kigeni wakiwasili Bandarini baada ya kuokolewa

Majeruhi wakipatiwa matibabu katika Hospitali ya Mnazi Mmoja




Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) imesema, meli iliyozama jana katika kisiwa cha Chumbe, Zanzibar ilikuwa na abiria 248 wakiwemo watoto 31. 

Kwa mujibu wa Sumatra, meli hiyo, inamilikiwa na Kampuni Seagul Transport, imasajiliwa na Mamlaka ya Usafiri Baharini Zanzibar (ZMA) na kwamba, Cheti cha Ubora kimeanza tarehe 24 Agosti, 2011 na kinamalizika 23 Agosti, 2012. Imesema, meli hiyo ilikuwa imeruhusiwa kubeba abiria wanaoruhusiwa 300 na tani 26 za mizigo.

SUMATRA kupitia Kituo cha Utafutaji na Uokoaji (MRCC) ilipata taarifa kuwa meli ya MV Skagit iliyokuwa safarini kutoka Dar es Salaam kuelekea Zanzibar ilikuwa inazama katika eneo la karibu na kisiwa cha Chumbe, Zanzibar, eneo ambalo lipo umbali wa Kilomita za Bahari 13.8 kutoka Bandari ya Zanzibar.

Zoezi la uokoaji linaendelea katika eneo la tukio kutoka kwa Mv Flying Horse, Mv Kilimanjaro III, Tug Bandari ya Zanzibar, KMKM, Mv Zanzibar I, Police Patrol Boat, Navy.
Taarifa hizi ni kwa mujibu wa vyanzo mbali mbali.

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII