HABARI MPYA LEO  

Airtel Yachangia Damu

By Unknown - Jun 29, 2012





kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imeandaa
zoezi la kuchangia damu litakalohusisha wafanyakazi wake kuchangia damu kwa lengo la kuokoa maisha ya wagonjwa wanaohitaji damu, hii ni moja kati ya shughuli za Airtel katika kusaidia jamii

Akiongea wakati wa zoezi la kutoa damu lililofanyika katika makao
makuu ya Airtel Mkurugenzi Rasilimali watu Perece Kirigiti alisema "Airtel inandeleza dhamira yake ya kusaidia na kuchangia katika shughuli za kijamii na leo tunashirikisha wafanyakazi wetu kuchangia damu katika kukiwezesha kitengo cha damu salama cha taifa kuwa na hifadhi ya damu ya kutosha kukidhi mahitaji ya wagonjwa na kuwezakuokoa maisha ya wagonjwa".

Tutakuwa na zoezi hili siku nzima ya Alhamisi hapa Ofisini makao makuu Dar es salaam ambapo madaktari kutoka kitengo cha taifa cha kutoa damu wataendesha zoezi la kutoa damu kwa wafanyakazi na wageni watakaojitolea kuchangia. Wafanyakazi wetu wanayofuraha kuona wanaokoa maisha ya watanzania nchini na kwa jinsi hiyo tunatimiza majukumu yetu katika kusaidia jamii inayotunzunguka.

Kwa upande wake Meneja huduma kwa jamiii bi Hawa Bayumi akichangia kuhusu jitihada hizi alisema” hii ni moja kati ya jitihada zetu za kuwawezesha wafanyakazi wetu na wadau mbalimbali kuona jukumu lao katika kusaidia jamii, na kwa mwaka huu wito ni changia damu ili kuokoa maisha”.

Zoezi zima la utoaji damu litahusisha kujaza fomu, mahojiano na uchunguzi wa afya utakaofanywa kwa kufata kanuni za tiba, kisha kufatiwa na utoaji damu utakaochukua takribani dakika 10 ambapo mililita 450 za damu zinategeme kuokoa maisha ya mtu mmoja.Tanzania inahitaji kiasi cha damu cha unit 350,000 kwa mwaka kwa ajili ya huduma za dharura za tiba ambapo kwa sasa kitengo cha damu salama
cha taifa kinakusanya unit 115,000- 120,000 kwa mwaka hivyo kuwa na mapungufu ya kiasi cha unit 235,000.

kitengo cha taifa cha kutoa damukitengo cha damu salama cha taifa wa damu kwa mwaka huu wa 2012 na kufanya juhudi za kukusanya unit 180,000, hivyo inatoa wito kwa watanzania wenye afya walio na umri kati ya 18 na 65 na uzito wa 50kgs kuchangia damu ili kuokoa maisha
ya wagonjwa wanaohitaji kuongezewa damu.
Maganga Media

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII