HABARI MPYA LEO  

Miujiza inawezekana; Evra

By Maganga Media - May 13, 2012

Patrice Evra
Patrice Evra-ana imani
Beki na nahodha wa klabu ya Manchester United Patrice Evra bado ana imani klabu yake inaweza kuondoka na ushindi wa Ligi kuu.


United, ikiwa katika nafasi ya pili kwa tofauti ya magoli tu, inahitaji kuiona City ikijikwaa dhidi ya QPR au uwezekano wa kuimiminia Sunderland mabao yasiyopungua tisa ili kuiondoa City kileleni kwa hio tofauti ya magoli manane.


Evra anasema, huenda watu watadhani nimechanganyikiwa, lakini ni imani niliyo nayo.


"naelewa kua hatma ya matokeo haimo mikononi mwetu. Lakini ikiwa tunataka kubaki na imani ya miujiza lazima tuishinde Sunderland."

Follow Maganga Media on Twitter, Feel free to like and comment Facebook. Stay updated via RSS

ANDIKA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII